Siku Ya Bwana
1Rafiki wapendwa, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua zote mbili nimejaribu kuziamsha nia zenu safi kwa kuwakumbusha mambo haya. 2Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa zamani na manabii watakatifu na ile amri ya Bwana na Mwokozi mli yopewa na mitume wenu. 3Kwanza kabisa ni lazima muelewe hili: kwamba siku za mwisho watu wenye dhihaka watakuja kuwadhihaki wakiwa wametawaliwa na tamaa zao wenyewe. 4Watawaambia, “Ali yeahidi atakuja yuko wapi? Tangu baba zetu walipokufa mambo yam eendelea kuwa kama yalivyokuwa tangu kuumbwa kwa dunia.” 5Wao wameamua kusahau kwamba ni kwa neno la Mungu mbingu zilikuwepo tangu zamani, na kwamba ulimwengu uliumbwa kutokana na maji kwa njia ya maji, 6na kuwa kwa maji hayo hayo ulimwengu ule uliokuwepo uliangamizwa wakati ule wa gharika. 7Lakini kwa neno hilo hilo mbingu na dunia, ambazo zipo hivi sasa, zimewekwa akiba kuchomwa moto, zimewekwa mpaka siku ile ya hukumu na ya kuangami zwa kwa watu wasiomcha Mungu.
8Lakini wapendwa msisahau neno hili, kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja. 9Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake kama watu wengine wanavyochukulia kukawia, bali yeye anawavumilia, maana hapendi mtu ye yote aan gamie, bali wote waifikie toba.
10Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Ndipo mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; na vitu vya asili vitateketezwa kwa moto na dunia na vitu vyote vilivyomo humo vitateketezwa.
11Kwa kuwa kila kitu kitateketezwa hivyo, ninyi je, mna paswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi maisha ya utaka tifu na utauwa, 12mkingojea na mkiharakisha kuja kwa siku ya Mungu, siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kutoweka, na vitu vyote vilivyomo ndani yake vitayeyushwa kwa moto! 13Lakini kufuatana na ahadi yake, sisi tunangojea mbingu mpya na dunia mpya ambamo haki huishi.
14Kwa hiyo wapendwa, kwa kuwa mnatazamia mambo haya, jita hidini ili mkutwe hamna doa wala lawama, mkiwa na amani naye. 15Hesabuni uvumilivu wa Bwana kuwa ni wokovu, kama ndugu yetu mpendwa Paulo alivyokwisha kuwaandikieni kwa hekima aliyopewa na Mungu. 16Ameandika hivyo hivyo katika barua zake zote akizun gumzia mambo haya. Barua zake zina mambo mengine ambayo ni magumu kuelewa, ambayo watu wajinga na wasio na msimamo huyapotosha, kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko; na hivyo wana jiletea kuangamia.
17Basi, ninyi wapendwa mkijua haya, jihadharini msije mka potoshwa na makosa ya hao waasi na kupoteza uthabiti wenu.